MESSAGE


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, October 24, 2012

KIJITO YETU WIKI ILOPITA

Mfululizo wa matukio yanayojiri katika Ibada K.K.K.T Kijito unaendelea, Wiki ilopita Ibada ya Kijito iliongozwa na Mch. Ernest Kadiva na Aliyesimama kwa ajili ya mkate wa kiroho alikuwa msaidizi wa Askofu, Mchungaji George Fupe ambaye alisisitiza watu kumtolea Mungu kwa moyo tunapoelekea katika kipindi cha mavuno tarehe 4 Novemba 2012. Katika ibada hiyo pia iliyopambwa na Praise Team walioongoza kipindi cha sifa na kuabudu.
Praise Team wakiongozwa na Allen Mwaipaja wakati wa kipindi cha PnW

Wapedwa wako busy katika kuabudu

Msaidizi wa Askofu, Mch Geoge Fupe akihubiri

Wadau wakapata nafasi ya kuombewa kabla hawajaanza maisha mapya ya ndoa, Tokea kushoto ni Bi Orpah Kiondo na mtarajiwa wake Elisha Mushaija na kulia ni Cuthbert Kagirwa na mke wake mtarajiwa

Wakapewa wazazi wa kiroho wa kuwa-guide katika maisha mapya

Kwaya ya vijana toka Azania Front wakiimba wakati wa ibada

No comments:

Post a Comment