MESSAGE


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, December 1, 2010

Monday, November 22, 2010

Kwaya ya Uinjilisti Kijito Yafanya Maandalizi ya Uzinduzi

Jumapili ya jana tarehe 21 Oktoba 2010, Kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama ilifanya maandalizi ya uzinduzi wa Album yao mpya Ijulikanayo kama NDANI YA SAFINA. Walivaa T-shirts zenye rangi na majina mbali mbali ya album walizowahi kuzitoa. Ikiwa ni pamoja na Hakuna Mwanaume Kama Yesu, Hakuna Mungu Kama Wewe, Twaokolewa kwa Neema na Ndani ya Safina. Kwa habari zilizopatikana toka kwaya hiyo. Wanategemea kuzindua album yao hiyo tarehe 28 ya mwezi huu yaani jumapili ijayo. Uzinduzi huo utafanyika katika kanisa la KKKT Kijitonyama katika ibada zote mbili. Na baadae mchana watakuwa na tamasha la uimbaji.

Haya ni matukio baadhi katika Picha










Thursday, November 18, 2010

Kwaya ya Uinjilisti Kijito Ziarani Mtaa wa Ununio

Jumapili iliyopita ya tarehe 14 Novemba. Kwaya ya uinjilisti ilipata kuhudumu katika mtaa mpya wa Ununio mtaa unaotunzwa na Usharika wa Boko. Wakiwa katika huduma ya kumtangaza kristo katika mtaa huo ambapo siku hiyo walikuwepo na viongozi wa kanisa akiwemo mkuu wa jimbo la kaskazini. Mchungaji Antha Muro na Askofu Gehazi Malasusa.
Lengo kuu lilikuwa kuuzindua jengo la ibada na harambee ya kuchangia umaliziaji wa jengo hilo. Makusudio yao ilikuwa kufikisha milioni 30. Kupitia "pledges" na vitu vilivyoletwa kunadiwa.

Angalia matukio kwa ufupi katika picha.
Hivi ndivyo linavyoonekana jengo la kanisa la mtaa wa Ununio! (ubavuni)

Hivi ndivyo linavyoonekana jengo la kanisa la mtaa wa Ununio! (Mbele)

Wakati Askofu Malasusa alipowasili mtaani hapo tayari kabisa kuianza ibada

Akielekezwa na mwenyeji wake (aliyemtangulia) Mchungaji wa usharika wa Boko.
Anayeonekana nyuma ni mchungaji Anta Muro Mchungaji na mkuu wa jimbo la kaskazini

Hawa ni baadhi ya wanakwaya wa kwaya ya uinjilisti kijito waliokuwepo.

Toka shoto ni Rosemary, Gift na Jacob nao walikuwepo, ni miongoni mwa wanakwaya
wa kwaya ya uinjilisti Kijito

Askofu akisisitiza jambo wakati wa mahubiri siku hiyo.

Bwana Aminiel Mushi akiwa katika kazi ya kunadi bidhaa mbali mbali zilizokuwepo

Kwa msisitizo akinadi Bw. Mushi

Akiifunga ibada ya siku hiyo na kutoa baraka kama anavyoonekana Askofu Malasusa
akiwa na watumishi wenzake. Akiwemo Mchungaji wa Usharika wa Kawe (Kulia)

Askofu malasusa akipozi kwenye picha

Hii ni picha ya pamoja askofu aliomba kupiga na washarika wote wa mtaa wa ununio!

Monday, November 8, 2010

KKKT- Kwaya Kuu ya Usharika wa Kijitonyama

Vijana wa Usharika Waweka Mikakati ya Kujikwamua

Jana jioni vijana wa KKKT usharika wa Kijitonyama, Walipata muda wa kukaa na kuzungumza mambo mbali mbali yahusuyo mambo yao. Miongoni mwa mikakati waliyonayo. Ni kuhakikisha kila kijana wa kanisa anamjua Mungu. Lakini pia kushiriki katika mambo mbalimbali ya jamii ikiwa ni pamoja na michezo, Kujifunza vyombo mbalimbali vya muziki. Na mengine mengi ikiwa ni pamoja na mipango ya kujikwamua kiuchumi. Kwa kuanzia vijana wameanza kwa kujisajiri kupitia fomu, simu ya mkononi, Pia kwa internet ambapo website itatoka hivi karibuni.

Fuatana nami uone matukio katika picha


Brain Storming!!
Katibu wa Vijana wa usharika, Bi. Neema Mrema akiwa busy kuchukua notes
Kwa pamoja kila mtu akitafakari nini azungumze ilimradi tu kufanikisha mipango
Mshiriki mmojawapo na kiongozi wa Felowship akichangia jambo.

Mzee wa kanisa kijana, Bw. Renard Shayo akisisitiza jambo.
Baade walipata mlo wa pamoja
Chakula kilipozidi kuwa kitamu automatically points zikaanza kupotea!!

Wednesday, November 3, 2010

Harusi Ya Emma na Stella

Nimepata malalamiko toka kwa wapenzi wa blog hii wakitaka waone japo picha za harusi ya Emma na Stella ilivyokuwa. Nami sikufanya kusudi nikaingia mtaani japo kusaka chache. Hebu na tuziangalie wote!!!


Wapambe wa kike walionekana hivi jamani. Walipendeza sana!

Wakati wakiingia kanisani kwa mwendo wa madaha!

Kijana anasema kimoyomoyo leo ni leo jamani. Mungu ameniona!

Furaha inapoongezeka Dada Stella Aamini amini kama ni kweli ndo
siku ya harusi yake!

Pale lilipotoka tamko kwa mchungaji akisema. Ni nani anamtoa Stella kwenda
kwa Emmanuel? Baba wa watu kwa upole ikabidi ajitose kutamka neno!

Kijana alipokabidhiwa kifaa wacha furaha imjae kama vile kashukiwa na roho
mtakatifu siku ya pentekoste. Ilikuwa kidogo tu aanze kunena kwa Kisambaa!

Ni kama wanasema... Tulimaanisha ngoja tuwaoneshe kweli tulidhamiria.

Baraka naziwe juu yenu mnapoyaanza maisha mapya ya ndoa. Vijana
wakakomba mibaraka kibao toka madhabahuni! Ikawafurika mpaka myoni!

Hapa sisemi.... Angalia mwenyewe!!!

Punde tu Emma akapata ajira ya ulinzi........
anaangalia kushoto na kulia kama usalama upo maana ameshamiliki
so lazima ahakikishe usalama upo na amlinde!


Jamani si mnaona wenyewe? Wametimiza ndoto yao. Hebu njooni wapongezeni

Hongereni sana, mmetutia moyo wazee wenu! Tunawatakia maisha mema!

Mashosti nao wamo kupamba msafara!

Hapa wanatoka kanisani kwa furaha nyingi!

Tarumbeta walikuwepo kushughulisha shughuli ikaenda uzuuuuuri kabisa!

Sauti ndogo inatoka.... Hivi Stella unajua nakupenda mke wangu? Nae anajibu
huju ameinamisha kichwa. Mmmmmh! najua sinimeona?

WAMEPENDEZA HAWAJAPENDEZA?