MESSAGE


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, May 28, 2012

TAMASHA LA KUCHANGIA USIKIVU MZURI WA RADIO YA UPENDO LAFANA

 Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akikabidhi mchango wa sh. mil. 10 kwa Mchungaji George Fute ambaye ni Msaidizi wa Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT,Askofu Alex Malasusa wakati wa hafla ya kuhitimisha harambee ya kuboresha usikivu wa Redio ya Dini ya Upendo 107.7 FM yenye lengo la kuchangisha na kupata kiasi cha sh. Mil. 220 iliyofanyika leo kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee,Jijini Dar es Salaam.
 Mchungaji George Fute ambaye ni Msaidizi wa Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT,Askofu Alex Malasusa akitoa shukrani kwa Mgeni wa Heshima katika hafla hiyo ambaye ni Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa mara baada ya kukabidhi mchango wake pamoja na marafiki zake wa sh. Mil. 10 kwa ajili ya kuboresha na kuongeza wigo mpana wa kusikika kwa Redio ya Upendo FM.

Mheshimiwa Edward Lowasa mgeni maalum akisalimiana na Askofu mstaafu Elinaza Sendoro wa K.K.K.T

 Mh. Lowassa akiongoza zoezi zima la uchangishaji wa fedha kwa watu mbali mbali waliofika ukumbini hapo kw ajili ya kuichangia Redio Upendo FM. 
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akitoa hotuba yake fupi kabla ya kukabidhi mchango wake na kuongoza harambee hiyo iliyofanyika leo kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee,Jijini Dar es Salaam.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akimpongeza Mwanamuziki wa Ijili kutoka nchini Kenya,Sarah K ambaye alishirikiana nae katika zoezi la kuchangisha fedha hizo.
 Mchungaji George Fupe ambaye ni Msaidizi wa Askofu Mkuu wa Kanisa la KKKT,Askofu Alex Malasusa akizungumza machache kwenye hafla hiyo kwa niaba ya Askofu Mkuu ambaye hakuweza kufika kwenye hafla hiyo.
 Meneja wa Redio Upendo FM,Agatha Lema akisoma hotuba katika hafla hiyo.
 Meneja wa Redio Upendo FM,Agatha Lema akiikabidhi hotuba hiyo kwa Mgeni Rasmi.

 Muimbaji wa Muziki wa Injili kutoka nchini Kenya,Sarah K akiimba moja ya nyimbo zake katika hafla hiyo.
 Muimbaji wa Muziki wa Injili kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia Congo,Faraja Ntaboba akiimba moja ya nyimbo zake katika hafla hiyo.
 Muimbaji wa Muziki wa Injili ,Jennifer Mgendi akiimba moja ya nyimbo zake katika hafla hiyo.
Muimbaji wa Muziki wa Injili,Joshua Mlelwa akiimba moja ya nyimbo zake katika hafla hiyo.
 Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiwapungia waumini waliofika ukumbini hapo.
Kwaya Kutoka K.K.KT Azania Front
Kwaya toka K.K.K.T Vetenary
 Vikundi vya Kwaya mbalimbali. 
Bwana Lenard Shayo akiwa na wageni toka USA Jimbo la Michigan Nancy Buchkuski, Joan Patacony wakiwa na mdau Julieth Mutabiilwa
Watu mbalimbali waliofika katika tamasha hilo

picha kwa hisani ya michuzi blog

Kijito Jumapili ya Jana

Katika nyumba ya ibada ya Kijitonyama K.K.K.T Jana palikuwa hapatoshi kwa wingi wa neema zilizojaa kupitiliza katika vipindi vyote vya ibada. Ibada ambayo iliongozwa na Mch. Ernest Kadiva akishirikiana na mtheolojia pamoja na Mhubiri machachari huyu si mwingine bali Mwinjilisti Kayuni ambaye alihuburi habari za Roho Mtakatifu. Kwani jana kanisa hilo lilikuwa linakumbuka siku ya Pentekoste. Pamoja na Kikundi cha sifa yaani Praise Team zilikuwepo kwaya nyingine pia Ikiwa ni Uinjilisti Kijito pamoja na Kwaya Kuu ya Usharika. Mambo hayakuwa haba. Angalia matukio hayo katika picha.

 Kijana Allen Mwaipaja akiongoza Praise Team katika kusifu na kuabudu

 Kanisa wakiwa katika hali ya kumsifu Mungu

 Kwaya ya Uinjilisti wakimsifu Mungu

 Kwa mbali anaonekana mamaNancy Buchkuski na rafiki yake Joan Pataconi na mzee Leonard Shayo wakicheza Ndani ya Safina.

 Mambo ya Kantate Domino tumwimbie Mungu kwa makabila yote, Jana ilikuwa siku ya Wahaya kumwimbia Mungu kwa lugha yao.

 Katibu wa Barala la wazee Kijitonyama mama Victoria Kisyombe akiwatambulisha wageni toka Usharika rafiki wa Kijitonyama, Unaoitwa Our Saviours Lutheran Church. Aliye katikati ni mama Nancy Buchcuski akiwa na rafiki yake Joan Pataconi wamekuja kuwatembelea jamaa na marafiki.

 Katika picha ya pamoja na baadhi ya wazee wa kanisa, wakipokea zawadi mbalimbali walizotoa wageni hao

 Mwinjilisti Kayuni akihubiri kwa msisitizo

 Kwaya Kuu waliokuwepo jana, wakisikiliza kwa makini wakati ibada ndo inaelekea ukingoni

Mchungaji Ernest Kadiva akitoa neno la baraka wakati wa kufunga ibada.

Tuesday, May 15, 2012

TAMASHA LA KWAYA ZA UINJILISTI NA UAMSHO DAR ES SALAAM LAAMSHA NYOYO ZA WATU

Hapo jana katika jimbo la Kaskazini(zamani Kinondoni) la kanisa la Kilutheri dayosisi ya mashariki na pwani kumefanyika matamasha mbalimbali yanayoshirkisha kwaya za Uinjilisti na Uamsho(UKUU),moja ya vituo ilikuwa usharika wa Manzese jijini Dar es salaam ambako kwaya za Uinjilisti Sayuni kinondoni,Kijitonyama,Kawe,Hannanasifu,Mwananyamala na Manzese,  ziliweza kumsifu Mungu kwa pamoja huku kwaya tatu ambazo nazo zilipangiwa katika kituo hicho hazikufika.

Tamasha hili lilifunguliwa rasmi kwa maombi yaliyoongozwa na mchungaji kiongozi wa kanisa hilo la Manzese,kisha kufuatiwa na uimbaji uliofunguliwa na kwaya ya Uinjilisti Sayuni Kinondoni na kuhitimishwa na kwaya ya Uinjilisti Manzese, Kilichowavutia watu zaidi ni jinsi ambavyo kwaya ya Uinjilisti Kawe ambao kila kukicha wamekuwa wakiongeza kiwango cha uimbaji,zamani kwaya hii ilikuwa imepewa jina la utani kwa kuitwa wanajeshi kutokana na waimbaji wake wengi kuwa wanajeshi kutokana na eneo walipo.Kisha kwaya ya Uinjilisti Kijito ambao watu walipendezwa na namna ya mpangilio wao wa muziki ulivyokuwa mzuri lakini pia na uchezaji wao. Sayuni hawakuwa nyuma wakiongozwa na soloist wao Balisidya aliyekonga nyoyo za watu jinsi alivyokuwa akicheza na sauti. Umoja huo wa kwaya za Uinjilisti na Uamsho(UKUU)umekuwaa ukifanya matamasha mara mbili kwa mwaka,mwezi wa tano kwa kuzigawanya kwaya katika makundi na tamasha la mwezi wa nane kwaya zote zaidi ya 15 zinakutana pamoja kwa uimbaji na kubadilishana vipawa.


 BAADHI YA MATUKIO KATIKA PICHA


Picha ya Kanisa la Lutheran Manzese baada ya ibada ya iliyofanyika asubuhi
 
Kwaya mbalimbali na washarika wakiwa tayari kwa tamasha


Wenyeviti wa kwaya mbalimbali zilizokuwepo wakitambulishwa na kiongozi wa UKUU


Mchungaji wa usharika akiongea neno la ufunguzi wa tamasha hilo









Waite Sayuni wazee wa Kinondoni ndio waliofungua tamasha
Wazee wa nguo za asili ndo wenyewe

Wanamuziki wa Kwaya hiyo wakiwa wanavicheza vyombo vyao vya muziki

Kwaya ya Hananasifu wakiwa jukwaani ndani ya BnW (Black and White)
Hawa ni Teule Mwananyamala ndio jina lao wakijishughulisha jukwaani
Katika mtizamo mwingine walionekana hivi

Fundi Mitambo Lukio Mjema akiwa kwenye mixer akiweka mambo sawa
 
Modest Mogan akiongoza sifa wakati wa matoleo

Uinjilisti Kijito wakisebeneka kwenye jukwaa

Jopo la wanamuziki wa Kijito wakivipapasa vyombo vyao

Anaye lead wimbo ni Gerald John, mwite Big ndo nick name yake ama (the voice)

Allen Mwaipaja akilitumia gunzi vema

Mwana dada Violet Mshiu wa Revocatus
 (aliyenyoosha kidole juu) akiimba kwa hisia

Shoto ni Eugene Mwamwembe akiwa na Kutyferra wakivicheza vinanda




Uinjilisti Kawe on the stage

Mwalimu Elidadi akiwaweka sawa waimbe kwa ustadi kama walivyolitawala jukwaa

Kawe wakiwa smart stejini

Hatimaye Calvary Manzese wakafunga dimba, 
Wanamuziki wa Manzese wakianzisha wimbo

Calvary Manzese kwa ujumla wao wakiwa kwenye steji

Washika magunzi wa Manzese wakifanya makamuzi