MESSAGE


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, July 9, 2013

Katika Ibada K.K.K.T Kijitonyama Wiki Hii

Katika ibada wiki hii, Kanisa la K.K.K.T Usharika wa Kijitonyama uwepo wa Bwana ukiwa umeshuka. Pale waimbaji walipomtukuza Mungu kwa nyimbo na mapambio. Yaliyoimbwa na kwaya mbalimbali zilizosali ibada hiyo ya tatu, Ikiwemo kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama, Kwaya ya UKWATA Dar Pwani - Kikundi cha mkoa. Pia ibada hiyo ikiongozwa na watumishi wengine akiwemo Mwinjilisti Kipingu aliyeongoza ibada akishirikiana na Parish worker wa Usharika wakati Mwinjilisti Roserine Kambeyi aliyehubiri habari za Kufunguliwa. Pia mtumishi huyu anaendesha semina ya neno la Mungu wiki nzima katika usharika wa Kijitonyama. Akiwafanyia watu maombi ya kufungulia toka nguvu za giza. Wenye mapepo na wagonjwa mbalimbali wakifunguliwa kwa jina la Yesu.

Habari katika picha:
 Mwinjilisti Leonard Kipingu akishirikiana na Parish Worker wakiongoza ibada

Kwaya ya UKWATA Dar Pwani - Kikundi cha mkoa wakimwimbia Mungu katika ibada. Vijana hawa ambao wamefanikiwa kutoa albamu yao "KAMA INAVYOONEKANA KWENYE PICHA HAPO CHINI" walikuwa wakiiuza cku hiyo baada ya ibada. Jipatie nakala yako umtukuze Mungu pamoja nao. Wasiliana nao kwa namba za simu zilizo hapo chini kwenye picha.

 Mwonekano wa CD ya Kwaya ya UKWATA Dar Pwani - Kikundi cha mkoa

 Na huu ndio mwonekano wa cover la albamu ya Kwaya ya UKWATA Dar Pwani - Kikundi cha mkoa

 Praise Team wakiliongoza Kanisa katika ibada ya kuabudu.

 Wanamuziki waliotumika katika ibada hiyo wakivipiga vyombo vyao katika hali ya kuabudu

 Upako unapowashukia wana muziki mambo huwa hivi, huku mafundi mitambo wakiwa busy kuweka mitambo sawa.

 Pichani anaonekana mama Anastazia Mujumba (Mwenye browse nyeusi) akimsikiliza Mwinjilisti alihudhuria yeye na jamaa yake pamoja na marafiki kumtukuza na kumshukuru Mungu kwa kutimiza miaka 80. Pamoja na shukurani hiyo mama huyo alimtolea Mungu shukrani kwa kazi za mikono yake. Pamoja na uzee huo lakini bado anweza kufanya kazi za mikono. Kulia ni mwanae Proscovia Mujumba.

 Mwinjilisti Kipingu akiomba baraka kwa Mama Anasatazia Mujumba

 Katika mahubiri huyu ndiye Mwinjilisti Roserine Kambeyi akijaa upako na nguvu za roho mtakatifu akihubiri habari za watu kufunguliwa toka vifungo vya mwovu shetani. Usikose kuhudhuria semina wiki hii.

 Mwinjilisti Kipingu akisoma Ujumbe wa mama Anastazia katika sadaka aliyoitoa uliosemeka... Hataka katika hali ya uzee huu, namshukuru Mungu anayeniwezesha kufanya kazi kwa mikono yangu"

 Hizi ni moja ya kazi anazozifanya mama Anasatazia, wakati zikinadishwa. Aliyeshi nguo tokea kushoto ni Everlight Matinga na bi Proscovia Mujumba

 Ikiwa imepita wiki moja baada ya harambee ya Kuchangia Mfuko wa Elimu katika Usharika wa kijitonyama. Watu walionekama kuendelea kuchangia mfuko huo kwa kuchukua kadi za bei mbalimbali zinazopatikana usharikani Kijitonyama. Huku wengine wakirudisha kadi hizo na pesa na kupewa risiti zao.
 
 Mhasibu wa Usharika Bw. Nicodemus Lekei aliyekuwa akitoa kadi hizo na kupokea fedha zilizochagishwa.

 Mwinjilisti Kipungu akisema neno la shukurani kuhairisha ibada hiyo