MESSAGE


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Sunday, August 19, 2012

Kijito Leo Hii 19 August 2012

Wapenzi wa K-junior Blog, Ni siku nyingine tena ya jumapili, kama kawida yetu huwaletea vipindi vya ibada inayofanyika kanisa la K.K.K.T Kijitonyama. Leo ilikuwa ni siku ya vijana hivyo ibada nzima iliongozwa na vijana. Ambao pia walijumuika pamoja na kwenda hospitali ya Mwananyamala kutoa huduma ya kugawa vitu kama Sabuni, Maji ya kunywa, Dawa za meno n.k. Pia kuadhimisha siku hiyo vijana walikusanyika pamoja kwa chakula cha mchana, Yafuatayo ni baadhi ya matukio ya siku hiyo katika picha.

 Kwaya ya uamsho ndio walitufungulia dimba

 Kwaya ya vijana wakafatia kumsifu Mungu

 Judith Munisi yeye alisoma neno.

 Abel Dilunga (a.k.a Gadi) Yeye alisoma matangazo

 Mtui (wa kwanza kulia) Leo alikaa high table a.k.a patakatifu pa patakatifu. Akiwa na mzee wa kukwea pipa Mwinjilist Kipingu

 Wadau Emmanule Sameji na my wife wake leo walitoa shukrani kwa mtoto wao Daniela kufikisha mwaka mmoja

 Wakipata baraka toka kwa mtumishi wa Mungu mwinji Kipingu

 Wadau wengine kibao walikuwepo kuwasindikiza

 Wakati wa sifa, duh! wacha we kisouth africa zaidi. Kitu cha Solly Mahlangu. Emmanuel kikitawala sifa

 Praise Team ya Kijito on the stage

 Wakati wa worship watu wakazama rohoni

 Praise Team wakimwandaa Mhubiri wa leo

 Huyu ndiye aliyetulisha chakula cha kiroho leo

 Wazee wa kanisa wa leo, wakifurahia jambo baada ya kumaliza ibada

Matarumbeta wakatuaga kwa wimbo.