MESSAGE


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, April 30, 2012

KKKT-DMP KIJITONYAMA WAZINDUA JENGO LA KITEGA UCHUMI

Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Dayosisi ya Mashariki na Pwani, Jana imezindua Jengo la ghorofa tisa lijulikanalo kwa jina la Kijitonyama Lutheran Centre sambamba na uzinduzi mwingine wa nyumba ya ghorofa moja ambayo usharika wa Kijitonya umeinunua nayo ikiitwa Kijitonyama Lutheran Centre Annex. Uzinduzi huo ulifanywa na Askofu mkuu wa Kanisa hilo Dr.Alex Gehaz Malasusa. Gharama za ujenzi wa jengo hilo kubwa na ununuzi wa nyumba hiyo umeligharimu kanisa hilo takribani shilingi za kitanzania bilioni 3.5 Jengo hilo litatumika kwa shughuli za kiofisi na nyingine kama zitakavyobainishwa na hapo baadae.
Katika uzinduzi huo ulioambatana na ibada askofu huyo aliwaasa wakristo kujitokeza kwa wingi katika kuchangia mchakato wa kupata katiba mpya. 
Fuatana nami kwa tukio hilo katika picha.

 Hilo ndilo jengo lililozinduliwa,Wanaoonekana kwenye picha ni wadau mbalimbali waliojihusisha katika kazi mbalimbali za kuhakikisha ujenzi hata uzinduzi unakwenda kama ulivyopangwa

 Huu ni upande wa kushoto wa jengo hilo

 Upande wa nyuma linaonekana hivi

 Maandamano yalioongozwa na kundi la wapiga tarumbeta, kuelekea kwenye jengo hilo kwa shughuli ya uzinduzi

 Watoto wa sunday school wa kanisa hilo nao wakiwa kwenye maandamano

 Wazee wa kanisa wakiwa na nyuso za furaha na wakiwa katika hali ya utanashati na kupendeza nao walihusika katika maandamano hayo.

 Parish wokers na watumishi wengine wa kanisa nao hawakuwa nyuma katika maandamano

 Wachungaji wa sharika mbalimbali nao wakiwa kwenye maandamano

 Na mwisho wa maandamano walikaa wakuu wa jimbo makatibu wa kuu pamoja na Askofu A.G. Malasusa

 Viongozi,waumini na vikundi vya kwaya wakiwa tayari wakisubiri uzinduzi wa jengo hilo

 Askofu Alex G. Malasusa akianza ibada ya uzinduzi wa jengo hilo

 Jopo la watumishi wa Mungu wakisikiliza kwa makini

 Kwa mbali ni kwaya aalikwa ya Winner toka Ubungo 

 Wazee wa kanisa nao wakiwa makini

 Parish wokers nao pia wakiwa katika hali ya uchaji

 Katibu wa baraza la wazee wa kanisa la Kijitonyama akisoma taarifa ya ujenzi wa jengo hilo

 Eng. Sanyiel Kishimbo aliyekuwa msimamizi wa ujenzi huo nae akitoa taarifa kabla ya kulikabidhi kwa katibu wa dayosisi

 Wakati ukafika na utepe ukakatwa tayari jengo likazinduliwa kelele za shangwe na vigelegele vikasikika

 Askofu akiwa amegusa lango kuu la jengo hilo huku akibariki kila aingiaye na kutoka katika mjengo huo

 Hii ni sehemu ya basement iliyomo ndani ya jengo hilo itakayotumika maalum kufundishia darasa la Sunday school kwa watoto wa kanisa hilo la Kijitonyama

 Watoto wakaonyesha furaha yao kwa kuimba wimbo wakifurahia sehemu ya ukumbi huo itakayotumika kama darasa kwao

 Hatua iliyofata ni ile ya kufungua sehemu ya jiwe la uzinduzi

 Askofu Malasusa akifungua sehemu ya jiwe la ufunguzi

 Jiwe la uzinduzi linaonekana hivi

 Hii ndiyo Kijitonyama Lutheran Centre Annex kabla ya kuzinduliwa

 Askofu Malasusa akizindua nyumba hiyo ya ghorofa moja kwa kukata utepe

 Watumishi mbalimbali ikiwa ni pamoja na wazee wa kanisa wakipozi katika picha ya pamoja

 Wachungaji wote waliokuwepo nao wakapozi katika picha ya pamoja

 Kwaya ya Winners toka Ubungo wakihudumu katika ibada

 Kwaya ya Umoja ya usharikani hapo wakihudumu katika ibada

 Askofu Malasusa akihubiri

 Hii ni kwaya ya uamsho, wakimwimbia Mungu wakati wa ibada

Tuesday, April 24, 2012

Tele-Seminar with Mwakasege

Mwalimu Christopher Mwakasege from Arusha,Tanzania, will not only teach, but also pray for all participants.
When?
Saturday, May 19
 
What Time?

    * USA & CANADA: 9am Central Time, 10am Eastern Time, 7am Pacific Time
    * ASIA:4pm Jerusalem / Israel Standard Time, 6pm Dubai, 7pm Karachi, 10pm Hong-Kong and Beijing; 11pm Tokyo
    * AFRICA:5pm Dar es Salaam, Kampala and Nairobi, 3pm Abuja, Lagos, Yaoundé and Kinshasa, 4pm Bujumbura, Lubumbashi and Kigali; 4pm Cape Town, Durban and Johannesburg; 14:00 GMT
    * EUROPE: 2pm London-UK, 3pm Rome, 4pm Sofia
    * AUSTRALIA: 1am Sydney

 How to log in:
 
Call: Tel: 218-895-2851 then enter Pass Code: 9102011
Due to the high volume of past callers, participants are advised to call in ahead of time. If your first attempt is not successful, do not give up. Keep calling until you get in! Prayers will start 30 minutes before the Seminar.
 
For more information about MANA MINISTRIES, please visit www.mwakasege.org  or Facebook: Christopher & Diana Mwakasege (Mana-Ministry)
 
Please share the details of this event with others!
 
MANA MINISTRIES USA & Tanzania
Tel: Toll Free: 1-888-481-6077 OR (651)334-0163 OR +255-27-2504289 (TZ) email: info@mikutano.com  Web: http://www.mikutano.com/ / www.mwakasege.org

HABARI NJEMA KWA WANA ICT (INFORMATION & COMMUNICATION TECHNOLOGY)

Rise And Shine For ICT Stakeholders In Tanzania

connectIt flier 600x400 Rise And Shine For ICT Stakeholders In Tanzania
There is a time when things seem to be going slow to the extent of making you lose focus on the purpose and importance of what you are doing. But you need to keep on doing it because that is what you have to do for survival.
Where is the fun, the enjoyment, the excitement ? Where is that driving force that kept you motivated throughout the day doing what you dreamed of being doing?
Does work have to be boring?
Hell NO! It is your choice to make it or kill, at least most of the time, unless you are working for the evil boss who does not have a clue about management.
Enough with all the boring stories, THE GOOD NEWS IS, If you are a Tanzanian ICT professional, student, enthusiast or doing whatever that goes along the lines of ICT, then you are in LUCK.
Qusaz intelligent solutions Ltd. is bringing to you “connectIT ICT conference 2012”  now, this is not just another ICT conference, NO! it is a very unique conference, brought to you by your fellow professionals in ICT, who have been experiencing the same things you have, who share the same thoughts, wishes and dreams about their careers and the ways to make them even better and FUN!

When? Where? What?

14th June 2012, This is THE date for connectIT conference, by the way I love the name “connectIT” sounds like connect it, but at the some time it sounds like connect information technology, any way enough with the name. The conference promises to have some of the best professionals in ICT as presenters, giving presentation on some very hot topics in ICT, security and measures to prevent the ever growing cyber attacks on apps, services and mobile transactions.
Usability and user experience in software and application design, methods, tips and ways to design applications for users, not machines. The new topics will be posted as the presenters confirms their statuses, so you need to sign up for the conference NOW
The conference will be held at Serengeti hall, Mbezi garden hotel in Dar es salaam Tanzania. on 14th June 2012.
DON’T MISS THIS WONDERFUL OPPORTUNITY 
connectIT conference website www.qusaz.com/connectit
Twiter @connectitz
On G+

 

Thursday, April 5, 2012

KIJITO WASHEREHEKEA SIKU YA MATAWI YA MITENDE

Jumapili hii ilikuwa ya aina yake, Pale usharika wa kijito uliposherehekea siku ya matawi ya mitende, habari za matawi ya mitende utazipata katika kitabu cha Yohana 12 Lakini kwa ishara tu jisomee hapa Yohana 12:13 wakatwaa matawi ya mitende, wakatoka nje kwenda kumlaki, wakapiga makelele, Hosana! Ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana, Mfalme wa Israeli! Kwa sifa na shangwe kubwa na mapambio washarika walimsifu Mungu na baadae kufuatiwa na ujumbe wa neno la Mungu uliotolewa na msaidizi wa Askofu Mch. George Fupe akisisitiza kuwa mtende ni alama ya uhai furaha na amani.


Jionee matukio katika picha kama yalivyochukuliwa na blogger wetu.


 Praise Team ya Kijito on the stage kwa furaha na matawi ya mitende juu kabisa wakiongozwa na Allen Mwaipaja


 Hawa ni baadhi ya wanakwaya wa kwaya ya Uinjilisti Kijito pamoja na wale wa kwaya ya Vijana Kijito wakisifu na kucheza wakati wa kipindi cha sifa 


 Sehemu ya washarika wakiwa katika hali ya kucheza na kusifu huku matawi ya mitende yakiinuliwa juu


 Kwaya Kuu nao hawakubaki nyuma katika kumsifu Mungu


 Kikundi cha matarumbeta (waliovaa pink) lakini pia Waziri Mkuu mstaafu wa pili kutoka kulia wakimsifu Mungu kwa pamoja


 Katibu wa baraza la wazee wa usharika wa Kijitonyama mwenye suti nyeusi na scarf nyekundu akiwa na uso wa furaha wakati wa ibada ya kusifu


 Msaidizi wa Askofu, Mch. George Fupe wakati akitoa neno huku akifundisha maana ya matawi ya mitende


 Kwaya Kuuu ya Usharika wakimsifu Mungu wakiongozwa na Mwl. Joachim Kisasa


 Michael Karata alitoa shukrani siku hiyo akimshukuru Mungu kwa mambo mengi ambayo Mungu amemtendea na katika kipindi kigumu alichopitia mke wake


 Waziri mstaafu Fredrick Sumaye akiwashukuru washarika wa Kijitonyama kwa kujitokeza katika harambee ya ujenzi wa usharika wake wa Makuruge


Mama Selina Mkonyi akiwahamasiha washarika kujitokeza na kuchukua fomu za kuchangia harambee ya kumalizia ujenzi wa kitega uchumi