MESSAGE


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, October 20, 2014

MTAA WA MABWEPANDE WAPATA WAZEE WAPYA

Ilikua ibada njema na ya furaha kwa wakazi  wa Mtaa wa Mabwepande hapo jana. Katika Kanisa la K.K.K.T Mtaa wa Mabwepande lililochini ya Usharika wa Kijitonyama. Wazee wapya walioteuliwa kusimama katika nafasi ya wazee wa mtaa huo, Waliwekwa wakfu na kuingizwa kazini na Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Kijitonyama Mchungaji Daniel Mbowe akishirikiana na Mwinjilisti Kamnde wa Mtaa huo jana waliongoza ibada hiyo walipowaaga wazee wa kipindi kichopita wa kuwakaribisha wazee wapya. Ibada hiyo pia ilihudhuriwa na kwaya ya Uinjilisti toka sharikani Kijitonyama pamoja na kwaya ya Uinjilisti ya Mtaa huo. Waliipamba ibada hiyo.

Kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama

Sehemu ya wazee walioteuliwa na washarika waliofika ibadani jana.

Kwaya ya Uinjilisti Mabwepande.

Wakati wa Neno Mchungaji Daniel Mbowe akihubiri


Kanisa lilifurika watu wengine wakaa nje.

Mzee aliyemaliza wakati wake akipokea zawadi ya cheti cha utumishi mwema.

Ndugu Eliasi Mboya akisoma neno.

Mchungaji Daniel Mbowe akiwaombea na kuwaweka wakfu wazee wapya walioteuliwa

Mwinjilisti Kamnde akisoma neno

Maombi yakiendelea

Kama wanavyoonekana wakati wa zoezi zima la kuwekwa wakfu wazee hao

Sehemu ya nje ya Kanisa hilo

Ndugu Kuttyferra aliteuliwa kusoma neno

Anociata Holela akisoma neno

Mchungaji Daniel Mbowe akiweka wakfu gari la Mwinjilisti Kamnde

Mwinjilisti Kamnde na familia yake wakizindua gari lao.

Gari hili limezinduliwa kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, AMEN

Bwana Mungu abariki kuingia kwenu na kutoka kwenu tangu sasa na hata milele. Ibada ikaisha hivo

Wednesday, July 2, 2014

KATIKA IBADA K.K.K.T KIJITONYAMA

Jumapili iliyopita tarehe 29-07-29-2014. Kama ilivyo ada ya Jumapili za mwisho wa mwezi usharikani Kijitonyama huwa na ibada ya Kusifu na Kuabudu na Maombezi. Ibada ya wiki iliyopita ilikua ya tofauti yenye kujaa nguvu za Mungu ndani yake. Ibada iliongozwa na Mchungaji Kiongozi wa Usharika Prosper Kinyaha akishirikiana na Mwinjilisti Leonard Kipingu pamoja na Mtumishi wa Mungu John Sembatwa aliyehubiri habari za Kuhuishwa na kutengenezwa upya lakini akisisitiza habari za kusamehe na kuachilia mambo uliyowahi kutendewa. Fuatana na mwandishi wa habari hizi katika picha hapo chini.

Praise Team wakishirikiana na Mtumishi wa Mungu Mwangosi (anayepiga keyboard) pamoja na wanamuziki wakiongoza washarika katika kuabudu.

Akina dada wa Praise Team wakiabudu

Akina kaka wa Praise Team wakiabudu

Kipindi cha sifa mambo ya Zambe wa Moyo!

Kanisa lilifurika sana watu walijaa, Kama wanavyoonekana wakijiachilia mbele za uwepo wa Mungu.

Kanisa likiwa limefurika watu mpaka ghorofani, Katika Ibada ya kusifu na kuabudu iliyofanyika siku hiyo.

Wengine walikosa mahali pa kukaa ndani ya kanisa, kama wanavyoonekana wakiwa kwenye hema lililokuwa nje ya kanisa.

Watu mbali mbali walimtolea Mungu shukrani zao za pekee kwa mambo makuu waliyotendewa, Mmoja wapo akiwa Grace Kaaya na binti yake (Waliopiga magoti Kulia).

Mchungaji Prosper Kinyaha, Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa K.K.K.T Kijitonyama akisema neno la Ukaribisho kwa Mtumishi wa Mungu John Sembatwa ambaye ndiye alihubiri siku hiyo.

Mtumishi wa Mungu John Sembatwa akiwa katika mahubiri.

Mchungaji Prosper Kinyaha na Mwinjilisti Leonard wakitoa neno la shukrani kwa Mtumishi wa Mungu John Sembetwa.

Monday, March 24, 2014

JUMUIYA YA EBENEZER YAWAJALI WAJANE

Katika ibada iliyofanyika jana katika Kanisa la K.K.K.T Kijitonyama. Ikiongozwa na Mchungaji Msaidizi wa usharika wa Kijitonyama Mch. Prosper Kinyaha akisaidiana na Bw. Onai Seng'enge aliyekua kiongozi wa ibada hiyo na Petro Zakayo ambaye ndiye alikuwa mhubiri.
Jumuiya Maalum (Ebenezer) al maarufu kama Jumuiya Mchanganyiko kwa umoja wao wakiwa wameshikilia jahazi la ibada hiyo jana waligusa nyoyo za wajane kwa kutoa sadaka ya Vyerehani vinne pamoja na vifaa vyote vya ushonaji kwa kundi la akina mama wajane wa usharikani hapo. Akisoma risala Bw. Daudi Goodluck Daudi Alisema wameguswa kufanyanya hivyo ili kuinua kipato cha akina mama hao. Aidha alisema takribani milioni moja na nusu zilitumika katika upatikanaji wa vifaa.

Matukio katika picha:

 Bwana Onai Seng'enge akiwa madhabahuni akiongoza Ibada.

 Mchungaji Prosper Kinyaha Mchungaji Msaidizi wa Usharika wa Kijitonyama

 Mchungaji Prosper Kinyama akiwaombea watu walikuja kumshukuru Mungu kwa shukrani za Pekee
Aliyewekewa mikono  mkono wa kulia ni kijana Francis Malya (Macha)

 Kwaya ya Jumuiya Maalum wakimtukuza Mungu wakati wa ibada

 Bi Everlight akiongoza jahazi la kwaya ya Jumuiya Maalum.

 Kijana wa Jumuiya Maalum akisoma neno la Waraka

 Kijana wa Jumuiya Maalum akisoma neno la Mahubiri

 Mwanadada huyu wa Jumuiya Maalum akisoma matangazo ya Usharika

 Petro Zakayo akihubiri

 Mchungaji Ernest Kadiva, Mchungaji Kiongozi wa Usharika wa Kijitonyama akitoa salamu.

 Bwana Daudi Goodluck Daudi Mwenyekiti wa Jumuiya Maalum akisoma Risala ya Jumuiya yao  Mbele ya washarika.

 Sehemu ya wana Jumuiya Maalum wakisikila kwa Makini wakati wa ibada.

 Maelfu ya watu waliofika kuabudu K.K.K.T Kijitonyama jana.

 Sehemu ya sadaka kwa wajane iliyotolewa na Jumuiya Maalum

 Tokea kulia mtu wa pili na wa tatu wakiwa wamejitokeza kuchangia sadaka kwa wajane

 Bi. Margaret Kamugisha akitoa tangazo juu ya Uchangiaji wa Huduma ya kupeleka Injili kusikofikika utakaofanyika katika Hotel ya Land Mark Ubungo tarehe 30/03/2014 Kuanzia saa nane Mchana.
Usikose mtu wa Mungu.

 Mwenyekiti wa Jumuiya Maalum Bw. Daudi Goodluck Daudi Akikabidhi kwa Mch. Ernest Kadiva, Sehemu ya vyerehani vinne pamoja na vifaa vya ushonaji vilivyotolewa zawadi kwa wajane wa Usharika wa Kijitonyama.

 Waonaonekana na nyuso za furana ni akina mama wajane wa Usharika wa Kijitonyama wakifurahia zawadi toka kwa Jumuiya Maalum baada ya kukabidhiwa zawadi hiyo na Mch. Ernest Kadiva.

 Hivi ndivyo ibada ilivyoisha kwa maombi ya pamoja.