MESSAGE


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, June 14, 2011

Mdau Isack Mrema Ala kiapo cha maisha!

Cherekochereko na nderemo vilisikia Katika Kanisa la KKKT-Mbezi Beach wakati mdau
Isack Mrema Alipokula kiapo cha kuwa na Bi Rosalia kwa maisha yake yote.
Na baadae sherehe kufanyika katika Ukumbi wa Budget Resort ulioko Kunduchi.



Kwa Habari zaidi BOFYA HAPA

Thursday, June 9, 2011

Kijito wiki hii

Wapenzi wa Blog hii. Naomba radhi kwa kuwacheleweshea matukio ya wiki iliyopita. 
Ni kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu. Nimewaletea matukio kwa njia ya 
video na matukio kwa njia ya picha yakuwa hewani muda si mrefu.

Yafuatayo ni matukio kwa njia ya video Utaona watoto wa Kijitonyama Sunday School
walivyoonesha kwa washarika jinsi walivyokuwa wamejiandaa kwenda katika tamasha la watoto lililofanyika jumapili iliyopita tarehe 5 June katika usharika wa Magomeni Mviringo. Pia utaona moja ya kwaya iliyohudumu kwenye ibada ya siku hiyo. Nayo si nyingine ni kwaya ya Uinjilisti ya usharika huo. Wakiimba wimbo wa nakimbilia msalabani.

Hivi ndivyo linavyonekana K.K.K.T Kijito


 Hivi ndivyo watoto wa Sunday School ya Kijito walivyoonesha vipaji vyao

 Mchungaji Kadiva akisema neno baada ya watoto kuimba

 Hatimaye waliombewa baraka ili wakauwakilishe vyema usharika

 Mdau Phesto Mwakyusa toka Ughaibuni akikabidhi zawadi kwa usharika toka ufini.

 Bwana Lenard Shayo alikuwepo kuzipokea akisaidiana ma mchungaji wa usharika

 Kwaya kuu ya usharika nao walikuwepo ndani ya nyumba

 Kwaya ya Uinjilisti wakihudumu ibadani siku hiyo

 Kwaya ya Uinjilisti wakiwa katika mtizamo mwingine


Nakimbilia Msalabani

 Haya sasa Ule wakati wa PnW (Praise and Worship) Ukiwa umeshika hatamu





 Mchungaji akisema jambo fulani kuhusu wadau hao. kama picha inavyosema

 Ndo ibado inaishiaishia hivyo

 Shoto ni Mwalimu Kisasa mtaalam na mwongoza uimbaji wa nyimbo hapo usharikani
 Mambo hayakuwa haba siku hiyo kijana Aggrey alipoamua kufunga ndoa

 Tabasamu la ukweli linaonekana jamani
 Anatafakari tu raha aliyonayo moyoni hakuna ajuaye ila yeye tu!

Step by step akiuelekea mlango wa kanisa tayari kwa ibada ya kufunga ndoa

Wednesday, June 1, 2011

Yaliyojiri Kijito Jumapili ya Tarehe 29 Mei 2011

 Jumapili ya wiki iliyopita ilikuwa ya baraka sana kwa Usharika wa Kijito. 
Pamoja na kuwa na ibada nzuri iliyojaa ratiba nyingi. 
Kwaya kuu ya usharika ilipata nafasi ya kuzindua album yao mpya
Mgeni rasmi wa shughuli hiyo alikuwa mh. Fredrick Sumaye waziri mkuu mstaafu. 
Pia baadae jioni
kulikuwa na tamasha la uimbaji uliozishirikisha kwaya za uinjilisti na uamsho jimbo la kaskazini (UKUU)
Fuatana nami katika matukio kwa njia ya picha

Waziri Mkuu mstaafu Fredrick Sumaye akikata utepe
 ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Album hiyo.


Kikosi  kazi cha kwaya ya Uinjilisti Kijito 
wakiwa tayari kwa kupanda jukwaani.

Washika magunzi nao hawakuwa nyuma 
katika kupaza sauti zao kumsifu Bwana Yesu

Kwa shangwe na furaha vijana wakipanda jukwaani kwa tabasamu
 kuubwa kabisa wakionyesha raha ktk Kristo

Kama uonavyo wakilipamba jukwaa.  Kweli ipo raha katika kumtumikia Mungu

Wakiwa wametulia tayari kwa kuanza uimbaji

Akionekana kwa mbali kijana Israel Mujumba akiliongoza 
kundi katika wimbo wa Nakimbilia msalabani.
Pendo Mwambungu a.k.a binti wa kuimba key za juu 
akiliongoza kundi kwa hisia za hali ya juu

Wanamuziki nao wakipiga vyombo kwa ustadi mkubwa.  
Tokea shoto ni Dr. Tuntufye akipiga bass guitar, 
Enock akiwa na rhythm, Micah Songo akilipiga solo
 na Kuttyfera akibofya kinanda 
Ni uimbaji kwa kwenda mbele

Kwaya ya Uinjilisti Ubungo

















Uamsho Kijito wakilipamba Jukwaa





Wazee wa kazi Sayuni kinondoni nao walikuwepo

Wapiga vyombo wa kwaya ya Sayuni wakiwa kazini

Mpiga kinanda wa Kwaya ya Uinjilisti Sayuni nae akionesha ustadi wake

Drummer Boy wa Sayuni akionesha Umahiri wake

Kwa kuangalia vazi tu utawajua hawa ni Sayuni wazee wa Kinondoni

Wakizipaza sauti zao ndani ya vazi la kimasai, Ilikuwa raha sana


Foma Foma akiwa na Drummer Boy wa Sayuni katika pozi