MESSAGE


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Monday, December 30, 2013

CVC WAFANYA SILVER JUBILEE

AIC Chang'ombe Vijana Choir jana wamefanya sherehe kubwa ya kuadhimisha miaka 25 tangu kuanzishwa kwa kwaya hiyo. Sherehe hizo zilifanyika kanisani kwao eneo la Chang'ombe Sokota. Katika ibada iliyosheheni kwaya nyingi ikiwemo kwaya ya AIC Shinyanga, AIC Dar es Salaam Choir, Neema Gospel Choir (AIC), Kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama, Kwaya ya Unjilisti Mtoni (Lulu), Kwaya ya Ukombozi toka K.K.K.T Msasani. Katika kuadhimisha miaka 25 ya kwaya hiyo pia walizindua jina jipya la kwaya yao na kuwa AICT Chang'ombe Choir na CVC kubaki kuwa Brand Name. 

 Watumishi wa Mungu walikuwepo na kuhudumu katika ibada hiyo.


 Kwaya ya watoto ya AICT Chang'ombe

 Kwaya ya wenyeji AICT Chang'ombe Choir



 Rose Jefa mwimbaji toka Kenya

 Kwaya ya Uinjilisti Kijitonyama

 Kwaya ya AIC Shinyanga 

 Wana LULU toka Mtoni

 MC Tito ndiye aliyeongoza jahazi 

 Keki ya miaka 25


 Hawa ni vijana wa kanisani hapo wenye umri wa miaka 25 waliobahatika kula keki hiyo.

 Mwenyekiti wa AICT Chang'ombe Choir akikata keki

 Walezi wa kwaya tangu kuanzishwa kwake

 Baadhi ya watunzi wa nyimbo zilizobeba albamu tangu kuanzishwa kwa kwaya hiyo.

 Askofu Salala akizindua jina jipya la AICT Chang'ombe Choir

Kikundi cha wagaratia wakipozi katika picha na watumishi wa Mungu

No comments:

Post a Comment