MESSAGE


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Tuesday, February 26, 2013

Maznat Bridal Care Kuazimisha miaka 10 ya utendaji kazi


Akizungumza na waandishi wa habari, Mkurugenzi wa Maznat Bridal Care bi Maza alisema. Tarehe 5 May 2013 itakuwa ni siku maalum ya kuadhimisha  miaka 10 ya Maznat Bridal Care.Sherehe hizo zitafanyika katika Ukumbi wa Diamond Jubliee uliopo Dar es Salaam.  Kampuni yake ambayo imekuwa ikijishughulisha na urembo na upambaji wa maharusi, katika upambaji wa nywele za  maharusi wa kike, kusafisha kucha n.k
Katika kipindi cha miaka kumi tangu mwaka 2003 mpaka mwaka huu ameshapamba maharusi zaidi ya 10,000 ambao ni watu wa vipato vya aina tofauti tofauti kuanzia wale vipato vikubwa iikiwa ni pamoja wale wasio kuwa na nguo za harusi aliweza kuwapamba na kuwapa nguo harusi  bure. Katika idadi hiyo ningependa wafike walau maharusi wa kike 800 tu ambao walipambwa na salon yangu wakati wa sherehe au harusi zao.

Siku hiyo watakuwepo wajasiriamali wane wakionesha bidhaa zao ambao tungependa wainuke na kuwa wajasiriamali wakubwa kabisa wakianzia chini na hatimaye kutimiza ndoto na matamanio yao. Matamanio ya Maznat Bridal Care kwa wajasiriamali washuhudie kwamba ukinia inawezekana, ili mradi uwe umejipanga na pia uwe mwaminifu kwa Mungu na kwa watu pia. Wito we tu ni “If You Can Dream it, You Can do it’’ Kama unaweza kuwa na ndoto za kufanya kitu, Unaweza kukifanya. Tutazindua Health andBeauty Workshops (Semina za Afya na Urembo) zitakazokuwazikifanyika mara 2 kwa mwaka katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Arusha na Mwanza.
Kwa upande wa burudani, zitakuwepo za muziki kwa watu wa aina zote, Atakuwepo mzee Yusufu, Bahati Bukuku, The Voice na THT.


Katika kuhakiki siku inapendeza kutakuwa na sare maalum ya kitenge toka Ghana kwa kila mgeni atakayefika ukumbini hapo, atapaswa kuwa amevalia sare hiyo. Kitenge hicho kitapatikana ukinunua tiketi yako mapema

Aidha siku hiyo zitatolewa zawadi mbali mbali kwa maharusi ambao walipambwa na salon yake, zawadi hizo zitawalenga wale ambao wamesha zaa watoto watatu katika kipindi cha mwaka 2003 hadi 2009 na wawe wanaweza kuvaa nguo walizovaa siku za harusi zao (Shela) na ziwakae vizuri pia wawe na na picha za nguo hiyo ikionekana vizuri walipozivaa siku ya harusi.
Pia zawadi nyingine za (shela)  3 zenye thamani ya shilingi za kitanzania laki 9 kila moja zitatolewa kwa bibi harusi watarajiwa, ambao watanunua tiketi maalum na kufanyiwa mchakato na ndipo wataibuka maharusi watatu tu na kupewa zawadi hizo.


 Sehemu ya wafanyakazi katika salon ya Maznat Bridal Care wakiendelea na kazi zao

 Hii ni sehemu ya mapokezi kama inavyoonekana kusheheni bidhaa za mapambo ya nywele

 Christian Bloggers wakisikiliza kwa makini maelezo toka kwa mmiliki wa salon ya Maznat Bridal Care

 Sehemu ya duka upande wa maua ya aina mbali mbalimbali kama yanavyoonekana kwenye display cabinet 

 Duka la vifaa vya upambaji wa maharusi lililopo eneo la salon hiyo 

 Katika duka hilo pia zinapatikana nguo za maharusi wa kike ( Shela)

 Waandishi wa habari za blog za kikristo (Christian Bloggers) 
wakiwa wamepozi katika picha ya pamoja

 Christian Bloggers wakitembelea duka hilo



No comments:

Post a Comment