MESSAGE


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, February 6, 2013

KIJITO KWAYA ZIARANI KKKT KITUNDA RELINI

Kwaya ya Unjilisti imefanya ziara ya kiinjili katika kanisa la K.K.K.T Kitunda Relini kwa Mch. Ibrahim Gibore walipofanya huduma ya kusifu na kuabudu katika ibada iliyoandaliwa na usharika huo. Wakihudumu pamoja na kwaya wenyeji za usharika huo. Waliipamba ibada kwa sifa moto na kuabudu kulikosababisha uwepo wa Mungu kushuka katika ibada hiyo. Aidha katika ibaya hiyo alikuwepo mwanamuziki wa injili Upendo Nkone aliyehudumu ibadani pia. Somo la siku hiyo lilikuwa wimbo wa Musa na wimbo wa Mwana Kondoo kama lilivyohubiriwa na Mch. Ibrahimu Gibore.

Haya ndiyo yaliyojiri katika picha

 Aliyeshika kipaza sauti ni Katibu wa kwaya ya Uinjilisti Kijito Bw. Manyiga akitoa salamu za kwaya kwa washarika, kushoto ni Mchungaji wa usharika Ibrahimu Gibore wa Usharika wa Kitunda Relini.

 Tokea shoto ni Allen Mwaipaja pamoja na Modest Mogan wakiwa kiroho zaidi wakati wa kipindi cha kuabudu wakati wa ibada

 Dada Upendo Nkone akiwa amewainua watu juu kwa sifa

 Hivi ndivyo hali ilivyokuwa upako wa sifa ulipowashukia wana wa Mungu

 Jopo la wanamuziki wa kwaya ya Uinjilist Kijito, Tokea kushoto Ni Jacob Mwaipaja akishughulika na gitaa la solo akifuatiwa na Micah Songo yeye akililazimisha gitaa la solo kutoa sauti kwa ustadi na anayefuatia ni Petro Mwampashi akiliungurumisha gitaa lenye mvumo mkuwa la bass

 Fundi mitambo Lukio Mjema kama kawaida yake ni kuhakiki Sound imekaa vizuri

 Sehemu ya umati wa washarika waliofika kuabudu kanisani hapo siku hiyo

 Kijana Michael Piniel akikipapasa kinanda huku pembeni mwake MC Foma foma akishindwa kujizua kwa upako uliomshukia. Alikuwa kiroho zaidi

 Kwaya wakiwa katika hali ya kuabudu na kuuita uwepo wa Mungu

Sifa inapokolea mambo huwa design hii

No comments:

Post a Comment