MESSAGE


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Thursday, April 5, 2012

KIJITO WASHEREHEKEA SIKU YA MATAWI YA MITENDE

Jumapili hii ilikuwa ya aina yake, Pale usharika wa kijito uliposherehekea siku ya matawi ya mitende, habari za matawi ya mitende utazipata katika kitabu cha Yohana 12 Lakini kwa ishara tu jisomee hapa Yohana 12:13 wakatwaa matawi ya mitende, wakatoka nje kwenda kumlaki, wakapiga makelele, Hosana! Ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana, Mfalme wa Israeli! Kwa sifa na shangwe kubwa na mapambio washarika walimsifu Mungu na baadae kufuatiwa na ujumbe wa neno la Mungu uliotolewa na msaidizi wa Askofu Mch. George Fupe akisisitiza kuwa mtende ni alama ya uhai furaha na amani.


Jionee matukio katika picha kama yalivyochukuliwa na blogger wetu.


 Praise Team ya Kijito on the stage kwa furaha na matawi ya mitende juu kabisa wakiongozwa na Allen Mwaipaja


 Hawa ni baadhi ya wanakwaya wa kwaya ya Uinjilisti Kijito pamoja na wale wa kwaya ya Vijana Kijito wakisifu na kucheza wakati wa kipindi cha sifa 


 Sehemu ya washarika wakiwa katika hali ya kucheza na kusifu huku matawi ya mitende yakiinuliwa juu


 Kwaya Kuu nao hawakubaki nyuma katika kumsifu Mungu


 Kikundi cha matarumbeta (waliovaa pink) lakini pia Waziri Mkuu mstaafu wa pili kutoka kulia wakimsifu Mungu kwa pamoja


 Katibu wa baraza la wazee wa usharika wa Kijitonyama mwenye suti nyeusi na scarf nyekundu akiwa na uso wa furaha wakati wa ibada ya kusifu


 Msaidizi wa Askofu, Mch. George Fupe wakati akitoa neno huku akifundisha maana ya matawi ya mitende


 Kwaya Kuuu ya Usharika wakimsifu Mungu wakiongozwa na Mwl. Joachim Kisasa


 Michael Karata alitoa shukrani siku hiyo akimshukuru Mungu kwa mambo mengi ambayo Mungu amemtendea na katika kipindi kigumu alichopitia mke wake


 Waziri mstaafu Fredrick Sumaye akiwashukuru washarika wa Kijitonyama kwa kujitokeza katika harambee ya ujenzi wa usharika wake wa Makuruge


Mama Selina Mkonyi akiwahamasiha washarika kujitokeza na kuchukua fomu za kuchangia harambee ya kumalizia ujenzi wa kitega uchumi





No comments:

Post a Comment