MESSAGE


I made this widget at MyFlashFetish.com.

Wednesday, June 1, 2011

Yaliyojiri Kijito Jumapili ya Tarehe 29 Mei 2011

 Jumapili ya wiki iliyopita ilikuwa ya baraka sana kwa Usharika wa Kijito. 
Pamoja na kuwa na ibada nzuri iliyojaa ratiba nyingi. 
Kwaya kuu ya usharika ilipata nafasi ya kuzindua album yao mpya
Mgeni rasmi wa shughuli hiyo alikuwa mh. Fredrick Sumaye waziri mkuu mstaafu. 
Pia baadae jioni
kulikuwa na tamasha la uimbaji uliozishirikisha kwaya za uinjilisti na uamsho jimbo la kaskazini (UKUU)
Fuatana nami katika matukio kwa njia ya picha

Waziri Mkuu mstaafu Fredrick Sumaye akikata utepe
 ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Album hiyo.


Kikosi  kazi cha kwaya ya Uinjilisti Kijito 
wakiwa tayari kwa kupanda jukwaani.

Washika magunzi nao hawakuwa nyuma 
katika kupaza sauti zao kumsifu Bwana Yesu

Kwa shangwe na furaha vijana wakipanda jukwaani kwa tabasamu
 kuubwa kabisa wakionyesha raha ktk Kristo

Kama uonavyo wakilipamba jukwaa.  Kweli ipo raha katika kumtumikia Mungu

Wakiwa wametulia tayari kwa kuanza uimbaji

Akionekana kwa mbali kijana Israel Mujumba akiliongoza 
kundi katika wimbo wa Nakimbilia msalabani.
Pendo Mwambungu a.k.a binti wa kuimba key za juu 
akiliongoza kundi kwa hisia za hali ya juu

Wanamuziki nao wakipiga vyombo kwa ustadi mkubwa.  
Tokea shoto ni Dr. Tuntufye akipiga bass guitar, 
Enock akiwa na rhythm, Micah Songo akilipiga solo
 na Kuttyfera akibofya kinanda 
Ni uimbaji kwa kwenda mbele

Kwaya ya Uinjilisti Ubungo

















Uamsho Kijito wakilipamba Jukwaa





Wazee wa kazi Sayuni kinondoni nao walikuwepo

Wapiga vyombo wa kwaya ya Sayuni wakiwa kazini

Mpiga kinanda wa Kwaya ya Uinjilisti Sayuni nae akionesha ustadi wake

Drummer Boy wa Sayuni akionesha Umahiri wake

Kwa kuangalia vazi tu utawajua hawa ni Sayuni wazee wa Kinondoni

Wakizipaza sauti zao ndani ya vazi la kimasai, Ilikuwa raha sana


Foma Foma akiwa na Drummer Boy wa Sayuni katika pozi

No comments:

Post a Comment